TFF YASIKITISHWA NA HALI YA SOKA LA ZANZIBAR



SHIRIKISHO la Soka Tanzania, linasikitishwa na hali ya uendeshwaji wa soka la Zanzibar baada ya kujitangaza kwa kamati ya muda ya uendeshaji ligi.
Akizungumza na wandishi wa habari jana,Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Jamal Malinzi amesema amesikitika kusikia kwenye radio watu wanajiita kamati ya muda ya uendeshaji wa ligi Zanzibar ikisema wametoa vifaa kwa klabu za Mafunzo na KMKM kwa ajili ya kujiandaa kwa mashindano ya kimataifa.
“Baada ya kusikia kuna kesi mahakamani tuliaiandikia ZFA barua yenye namba ya kumbukumbu TFF/ZFA-03/2015, tukieleza jinsi shirikisho linavyosikitishwa na kuwepo kwa kesi dhidi ya ZFA”.
Malinzi alisema awali baada ya kikao cha usuluhishi wa mgogoro wa ZFA kilichofanyika, Dar es Salaam chini ya Uenyekiti wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi baada ya kuwepo tishio la Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuifungia Zanzibar kwenye soka ya kimataifa baada ya kufikishana Mahakamani, jambo ambalo ni kinyume na sheria za FIFA. 
Pia katika kikao hicho Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), kiliagizwa kuitisha Mkutano Mkuu wa dharura kujadili mwenendo wa Kamati ya Utendaji na mambo mengine kadhaa ikiwa ni pamoja na kwenda kufuta kesi zote mahakamani jambo ambalo lilitendeka na kujibiwa kwa maandishi na ZFA.
Pia Malinzi amesema amemwagiza Katibu wa TFF, Selestine Mwesigwa kumwandikia barua Rais wa ZFA, Ravia Idarus, akimtaka amjulishe kama yeye ndiye anasimamia na kuendesha mambo ya soka visiwani humo ili waijulishe CAF waweze kuchukua hatua kwani ZFA ni mwanachama wa wake.
Klabu za Chuoni na Aluta ndizo zilizofungua mashtaki mahakamani wakimtuhu Rais wa ZFA, Ravia Idarus,Makamu wa ZFA toka Pemba, Ally Mohamed pamoja na Katibu Mkuu, Kassim Haji Salum kukiuka kanuni za mashindano.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Chapisha Maoni