
Portugal ilitawala mechi hiyo lakini mlinzi wa Bulgaria Leiria alikataa katakata kuwapisha washambuliaji wa Ureno.
Ronaldo ambaye alikosa penalti akiichezea Real Madrid dhidi ya Sevilla siku ya jumapili aliona mkwaju wake wa kipindi cha pili ukiokolewa baada ya Nikolay Boduro wa Bulgaria kuunawa mpira katika eneo la hatari.
Hatahivyo licha ya kushindwa kufunga penalti hiyo dhidi ya Sevila Real Madrid iliibomoa Sevilla mabao 4-0 katika mechi ya La Liga lakini penalti dhidi ya Bulgaria ilikuwa mwiba kwa Portugal kwa kuwa licha ya kushambulia mara 30 hawakuweza kufunga.
0 maoni:
Chapisha Maoni