Jonathan Mensah ajiunga na Anzhi Makhachkala

Jonathan Mensah 
 
Mlinzi wa Ghana Jonathan Mensah amejiunga na Anzhi Makhachkala katika mkataba wa miaka miwili u nusu.
Mlinzi huyo wa Black Stars mwenye umri wa miaka 25 alikuwa akiichezea Evian Thonon Gaillard katika mkataba uliofaa kukamilika mwisho wa msimu.
Atajiunga na Anzhi Makhachkala mwishoni mwa msimu wa baridi.
Mensah alikuwa miongoni mwa kikosi cha timu iliyoshinda kombe la dunia la vijana mwaka wa 2009.
Vilevile aliichezea Black Stars katika kombe la dunia mwaka wa 2010 na 2014.
Vilevile alikuwa katika timu iliyoiwakilisha Black Stars katika mashindano ya ubingwa wa Afrika mwaka wa 2010 na 2015.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Chapisha Maoni