Martin Jol achukua usukani Al Ahly Misri

Aliyekuwa kocha wa Tottenham na Fulham ya Uingereza, Martin Jol, ndiye kocha mpya wa klabu ya Al Ahly ya Misri.
Mholanzi huyo amerithi kiti kilichowachwa wazi mwezi januari mwaka huu na kuondoka kwa kocha mreno Jose Peseiro aliyeihamia Porto.
Kuwasili kwake mjini Cairo kunamaanisha kuwa mahasimu wa jadi katika ligi kuu ya Misri Ahly na Zamalek wote wanamakocha wapya.
Zamalek majuzi tu walimsajili kocha mpya Alex McLeish.
Kwa sasa Jol anawasili Ahly wakiwa kileleni mwa jedwali la ligi kuu ya Misri wakifatwa kwa karibu na mabingwa watetezi Zamalek.
Mbali na kuifunza Tottenham na Fulham, Jol vilevile ameifunza vilabu vya Ujerumani Hamburg na Ajax Amsterdam ya Uholanzi.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 60 amekuwa akishabikia mechi kupitia kwa runinga baada ya kibarua chake kuota nyasi mwaka wa 2013 alipofutwa kazi na Fulham.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Chapisha Maoni