FAINALI YA FA CUP INAZIKUTANISHA MAN UNITED VS CRYSTAL PALACE BAADA YA MIAKA 26

Palace
Crystal Palace itakutana na Manchester United kwenye mchezo wa fainali ya kombe la FA May 21 mwaka huu baada ya kupambana kupata ushindi dhidi ya Watford kwenye mchezo wa nusu fainali.
Yannick Bolasie alifunga goli kwa kichwa kwa upande wa Palace kwenye uwanja wa Wembley kutokana na mpira wa kona uliopigwa na Yohan Cabaye.
Watford wakicheza bila ya kiungo wao Etienne Capoue ambaye aliumia mapema kipindi cha kwanza, walisawazisha bao hilo baada ya Troy Deeney kukutana na mpira wa kona uliopigwa na Jose Manuel Jurado.
Palace walijihakikishia kucheza fainali ya FA Cup baada ya miaka 26 baada ya Connor Wickham kupachika bao la ushindi kwa kuunganisha krosi ya Pape Souare.
Mchezo wa fainali utakaochezwa mwezi ujao ni marudio ya ule wa mwaka 1990 ambapo Palace na United zilikipiga kwenye mchezo uliomalizika kwa sare ya magoli 3-3 kabla ya The Red Devils kushinda kwa bao 1-0 kwenye mchezo wa marudiano.
Pardew adhihirisha ubora wake
Kocha wa Palace Alan Pardew alishangilia filimbi ya mwisho kufuatia ushindi ambao timu yake ilistahili akiwa amewapumzisha wachezi wake nyota kwenye mchezo waliopoteza kwa kufungwa goli 2-0 na Manchester United.
Mashabiki wachache wa Palace ambao waliamini huenda timu yao ingefuzu kucheza fainali ya FA Cup baada ya Pardew kuichukua miezi 15 iliyopita ikiwa kwenye hatari ya kushuka daraja.
Alipambana na timu yake kufanikiwa kumaliza ndani ya top 10 msimu uliopita na sasa ameisaidia kuingia kwenye fainali ya FA Cup ambapo huenda wakatwaa kombe hilo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Chapisha Maoni