
- Paul Dybala $68.28m
Haishangazi kumuona kinda huyu mwenye kipaji katika orodha ya wachezaji 20 wenye thamani kubwa zaidi hivi sasa, Juventus inajivunia kijana huyu na hawapo tayari kumuuza hivi sasa kutokana na uwezo wake wa kucheza sehemu yeyote katika mstari wa mbele wa ushambulizi.
- Diego Costa $71.56m
Mshambuliaji huyu wa Chelsea amekua hana msimu mzuri tangu kuanza kwa msimu huu lakini fomu yake ya mwaka jana inamfanya aingie katika orodha hii ya wachezaji 20 wenye thamani kubwa.
- Romelu Lukaku $74.51m
Inakupa maswali mengi kwanini kocha Jose Mourinho alimuachia kijana huyu raia wa Ubelgiji mwenye miaka 22. Lukaku ameendelea kuzifumania nyavu akiwa na klabu ya Everton na hivi sasa anaongoza katika kinyang’anyiro cha ufungaji mabao nchini England.
- Gareth Bale $75.49m
Majeruhi yanayomuandama mchezaji huyu huenda yamechangia kuwa pamoja na kuwa ndio mchezaji aliyesajiliwa kwa gharama kubwa zaidi duniani, lakini thamani yake imepungua sana hadi sasa anashika nafasi ya 17. Anahitaji kupandisha gemu yake huku akibakia free injury ili arudi katika ubora wake.
- Robert Lewandowski $76.03m
Rekodi yake ya mabao akiwa na Bayern Munich msimu huu na uliopita unamfanya Mpoland huyu kuwa mshambuliaji hatari zaidi wa kati duniani.
- Thomas Muller $77.89m
Huyu ni pacha wa Robert Lewandowski katika safu ya ushambuliaji, rekodi zake za mabao akiwa Bayern na timu ya taifa ya Ujerumani inamfanya Muller kuwemo katika orodha hii.

- Kevin de Bruyne $79.75m
Kama ilivyo kwa Mbrazil Philippe Coutinho, Kevin de Bruyne ni moja ya wachezaji hatari zaidi katika mstari wa pili nyuma ya mshabuliaji. Haikua kazi kwa Manchester City kuilipa Wolfsburg pauni 54m kumnasa mbelgiji huyu.
- Paul Pogba 84.45m
Kiungo huyu wa Juventus na timu ya taifa ya Ufaransa, alitajwa katika kikosi cha wachezaji 11 bora duniani pamoja na akina Lionel Messi na Cristiano Ronaldo, ni miongoni mwa wachezaji wenye umri mdogo wanaozivutia klabu nyingi sana hivi sasa.

Usajili wake kujiunga na Manchester United tena kwa pesa nyingi zaidi akiwa na umri wa miaka 19 tu, ulitajwa na wengi kama kamali, kijana huyu hivi sasa, pamoja na United kutokua na msimu mzuri, Martial anaonesha kuwa msaada mkubwa Old Trafford.
- Alexis Sanchez $89.47m
Huwezi kuwataja wachezaji watatu muhimu zaidi katika kikosi cha Arsenal ukamuacha Alexis Sanchez. Raia huyu wa Chile anastahili kuwa katika orodha hii.
- Sergio Aguero $89.69m
Anaweza kuwa ndiye mchezaji bora zaidi wa muda wote wa klabu ya Manchester City, ana kila kitu mshambuliaji anastahili kuwa nacho.
- Luis Suarez $94.28m
Umoja wake na Lionel Messi, pamoja na Neymar katika kikosi cha Fc Barcelona, unamfanya Suarez kuwa miongoni mwa wachezaji wenye thamani kubwa zaidi hivi sasa.
- Antoine Griezmann $96.46m
Baada ya kuondoka kwa mastaa kadhaa kikosini Atletico Madrid, Mfaransa huyu anabakia kuwa tegemezi zaidi huku akifunga magoli karibu kila mechi.
- Raheem Sterling $98.10m
Ugumu wa usajili wake kutoka Liverpool, sanjari na pesa waliyoitoa Manchester City unaonesha thamani halisi ya Raheem.
- Harry Kane $99.74m
Ukitaka kujua thamani halisi ya kijana huyu mwingereza, ni pale utakapoamua kutaka kumsajili, ana kila kitu mshambuliaji anatakiwa kuwa nacho.
- Cristiano Ronaldo $124.54m
Amemaliza kila kitu, umri unasogea, moja kati ya wachezaji bora zaidi kuibariki dunia ya mpira.
- Eden Hazard $142.56m
Wengi tunaweza kushtushwa na jina la Hazard katika nafasi ya tatu, lakini tukumbuke kuwa thamani ya mchezaji inahusisha vitu vingi sanjari na uwezo uwanjani, lakini pia mauzo ya jezi n.k
0 maoni:
Chapisha Maoni